Maafisa Wilaya wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) wameshiriki katika uangalizi wa Uchaguzi Mdogo wa Udiwani kwa upande wa Tanzania Bara ambapo wagombea 127 kutoka vyama 18 vya siasa wameshiriki katika Uchaguzi Mdogo wa Udiwani katika kata 22 za Tanzania Bara, Uchaguzi uliofanyika tarehe 20 Machi, 2024.

Akitoa pongezi zake kwa Tume ya Uchaguzi ya Taifa (NEC) na wananchi waliojitokeza katika Uchaguzi huo Afisa Uchaguzi Wilaya ya Magharibi ‘B’ Khadija M. Ali, wakati wa kutembelea
Vituo vya Kupigia Kura Kata ya Kimbiji Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni Mkoa wa Dar-es-Salaam alisema wadau wote wakiwemo wapiga kura na wananchi katika kata hiyo wamefanya Uchaguzi kwa utulivu mkubwa na mwitikio wa wananchi katika kata hiyo umekuwa wakuridhisha.

Sambamba na Hilo ameipongeza Tume ya Uchaguzi ya Taifa NEC kwa kuwapa mualiko huo kwani unaendeleza mashirikiano mazuri na mema baina ya Tume hizo mbili katika masuala ya kitaifa yanayohusiana na Uchaguzi.

Nae Issa Juma Hamad Msaidizi Afisa Uchaguzi Wilaya ya Micheweni ambae alitembelea vituo vya kupigia Kura katika kata ya Msangani Halmashauri ya Mji Kibaha Mkoa wa Pwani pamoja na Mahmoud Ahmada kutoka Wilaya ya Mkoani aliwashauri wananchi kuendelea kujitokeza kwa wingi kupiga kura ili kutimiza haki yao ya kuchagua viongozi wanaowataka katika Uchaguzi huo wa Madiwani.

“wito wangu kwa Wapiga Kura wajitokeze kwa wingi kwenda kupiga kura kwa ajili ya kuchagua madiwani wetu ambayo kila”

Aidha, aliwaomba Wapiga Kura kutekeleza jukumu hilo kwa utulivu na amani kwani kuna maisha baada ya Uchaguzi huo Mdogo.

Katika uangalizi huo Maafisa 4 wameshiriki katika Uchaguzi huo ambao ni Msaidizi Afisa Uchaguzi wa Wilaya ya Kati Said H. Vuai na Afisa Uchaguzi Wilaya ya Magharibi ‘B’ Khadija M. Ali, Issa J. Hamad kutoka Wilaya ya Micheweni na Mahmoud A. Mbwana kutoka Wilaya ya Mkoani Pemba,

ZEC na NEC zimekuwa zikishirikiana katika masuala mbalimbali ya Kiuchaguzi kwa mujibu wa Kifungu cha 119 (14) cha Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984.

 

 

Mawasiliano Yetu


Tume ya Uchaguzi Zanzibar

S.L.P 1001 - Zanzibar, Tanzania.

Simu: +255 242231489

Nukushi: +255 242233828

Mitandao ya Kijamii