Leo tarehe 24 Januari 2024 Mkurugenzi wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar Ndugu Thabit Idarous aliikaribisha Kamati ya Bajeti ya Baraza la Wawakilishi inayotathmini utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo na programu mbali mbali za Serikal ikiongozwa na Mwenyekiti wake Mwanaasha Juma Khamis ambae ni Muwakilishi wa Jimbo la Dimani, kamati hiyo imetembelea mradi wa Ujenzi wa Afisi Kuu ya Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) Maisara,Mjini Unguja ulioanza rasmi tarehe 11 Januari mwaka huu na unatarajiwa kukamilika kwa kipindi cha miezi 9.

Ujenzi huo unasimamiwa na Kampuni ya Ujenzi ya CRJE kutoka China ambapo watajenga jengo la kisasa lenye Ghorofa nne ambazo zitajumuisha kumbi mbali mbali za Mikutano ikiwemo Ukumbi wa kutangazia matokeo ya Uchaguzi, Studio ya Redio na TV, Ghala la Kuhifadhia Vifaa vya Uchaguzi N.k

Jengo hilo linatarajiwa kuwa la Kisasa zaidi kuendana na hadhi ya Afisi za Tume nyengine Duniani.

 

Mawasiliano Yetu


Tume ya Uchaguzi Zanzibar

S.L.P 1001 - Zanzibar, Tanzania.

Simu: +255 242231489

Nukushi: +255 242233828

Mitandao ya Kijamii