JAALA MAKAME HAJI- ZEC

Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar imewaomba Wapiga Kura waliomo ndani ya Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kufanya maandalizi ya mapema kwa ajili ya kuhakiki taarifa zao muda ukifika ambapo kazi hiyo ya uhakiki itafanyika sambamba na kazi ya kuandikisha Wapiga Kura wapya katika daftari hilo kwa mujibu wa ratiba itakayotolewa na tume.

Akizungumza katika semina ya wanafunzi wa skuli za sekondari za wilaya ya Magahrib “A” Afisa Uchaguzi wa Wilaya hiyo ndugu. Ali Rashid Suluhu alisema wapiga kura wote watapaswa kuhakiki taarifa zao za kitambulisho cha mzanzibar mkaazi ambacho kitawawezesha kuhakiki taarifa zao katika Daftari la kudumu la wapiga kura kwani bila kuhakiki taarifa huwezi kupiga kura kwa Uchaguzi ujao.

Akizungumzia kuhusu uandikishaji wa Wapiga Kura Wapya ndugu Suluhu aliwata wazazi na walezi kuwahamasisha vijana ambao wamefikia umri wa miaka kumi nane ambao hawana vitambulisho vya Mzanzibar Mkaazi kufanya jitihada za makusudi kupata vitambulisho hivyo ili nawao waweze kuandikishwa kuwa Wapiga Kura muda ukifika.

Naye msaidizi Afisa uchaguzi Wilaya ya Kaskazini “A” Bi Miza Pandu Ali alisema, Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar itaweka wazi majina ya wapiga kura katika vituo vyote vya kujiandikisha baada ya kumaliza kazi ya uandikishaji wa wapiga kura wapya na uhakiki wa taarifa za wapiga kura waliomo katika daftari la kudumu la wapiga kura.

Bi Miza Pandu alifahamisha kwamba, lengo la kuweka wazi majina ya wapiga kura ni kuwapa fursa wapiga kura kujiridhisha kuhusu usahihi wa taarifa zao na kuweka pingamizi kwa wapiga kura ambao hawana sifa za kuandikishwa katika eneo husika.

Bi Miza aliongeza kusema kwamba, wakati wa zoezi la uandikishaji Tume haitofanya shuhuli za uendelezaji wa Daftari kwa wapiga Kura wanaoomba kubadilisha na kusahihisha taarifa zao pamoja na Wapiga Kura waliopoteza shahada zao na badala yake shuhuli hizo zitafanyika katika ofisi za Uchaguzi za Wilaya mara baada ya kukamilika kwa kazi ya Uandikishaji na uhakiki wa taarifa.

Kwa nyakati tofauti wanafunzi wa skuli za sekondari za Wilaya ya Magharib “A” wameiomba Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar kuendelea kutoa elimu ya Wapiga Kura ili kila mwananchi aweze kutumia haki yake ya kupiga kura muda ukifika.

Afisa Uchaguzi wa Wilaya ya Kaskazini A Ndg. BAKAR BURHANI SULEIMAN akizungumza na wanafunzi wa skuli ya sekondari ya Bububu katika mafunzo ya elimu ya Wapiga Kura juu ya Uandikishaji na uhakiki wa taarifa za Wapiga kura

Tume ya Uchaguzi imepanga kutoa elimu ya wapiga kura kuhusu uandikishaji na uhakiki wa taarifa za wapiga kura kwa wanafunzi wa skuli za sekondari 44 na taasisi za elimu ya juu 17 kwa wilaya zote za unguja na pemba.

 

 

Mawasiliano Yetu


Tume ya Uchaguzi Zanzibar

S.L.P 1001 - Zanzibar, Tanzania.

Simu: +255 242231489

Nukushi: +255 242233828

Mitandao ya Kijamii