Na Jaala Makame Haji-ZEC

Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar Mhe. Jaji Mkuu (Mst) HAMID MAHMOUD HAMID alisema Uteuzi wa wagombea wa kiti cha Urais unafanyika kwa mujibu wa maelekezo ya kifungu cha 26 cha Katiba ya Zanzibar, 1984 na kifungu cha 43 cha Sheria ya Uchaguzi Nam. 4 ya mwaka 2018.

Kauli hiyo aliisema wakati akitoa maelekezo ya ujazaji wa fomu za uteuzi kwa Wagombea waliofika kwa nyakati tofauti katika Afisi ya Tume ya Uchaguzi Maisara kwa ajili ya kuchukua fomu za kuomba kuteuliwa kwa nafasi ya urais wa Zanzibar kwa tiketi ya vyama vyao.

Mwenyekiti huyo alisema ili mtu ateuliwe na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar kuwa mgombea wa kiti cha Urais, atalazimika kuwa na sifa kwa mujibu wa Katiba na Sheria ya Uchaguzi inavyo elekeza.

Alisemaa kuwa, mgombea atalazimika kujaza fomu  ya tamko la maadili  ya  mwaka 2020  na tamko la  kutojihusisha na vitendo vya  rushwa na  hai ya kiapo  katika fomu  katika fomu iliyojazwa  na kutia saini  na  Mgombea  mbele  ya Jaji  wa Mahakama  kuu ya Zanzibar.

 

Wakizungumza   kwa nyakati tofauti baada ya kupatiwa fomu  hizo  na mwenyekiti wa ZEC wagombea hao walisema endapo watapata  ridhaa ya kuteuliwa na wananchi watahakikisha  wanaunga mkono juhudi za Serikali  na kuendeleza yale yote mazuri yaliyofanywa na  Serikali ya awamu ya saba  chini ya uongozi wa Dkt.Ali Mohamed Shein.

 

Walisema kuwa watahakikisha wanasimamia haki, kuimarisha uchumi  na kuandaa mazingira mazuri ambayo  yatatoa fursa  kwa vijana kusoma  hadi chuo kikuu bila ya malipo yoyote

Aidha, Wagombea hao waliahidi kuwa, wataendelea kushirikiana na  Tume   na Serikali katika kukubaliana  na maelekezo ya Uchaguzi pamoja na  kuridhia matokeo  ya  uchaduzi  yatakayotangazwa na Tume ya uchaguzi ya Zanzibar na Tume ya Taifa ya Uchaguzi.

Wagombea  walio kabidhiwa  fomu hizio ni pamoja na Mgombea wa chama cha ADA-TADEA  Mhe. Juma Ali Khatib, Mgombea wa NLD ndugu Mfaume Khamis Hassan na Mgombea wa ADC Mhe. Hamad Rashid. 

 

Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar kesho tarehe 28/8/2020 Mgombea wa Uraisi kupitia chama cha ukombozi wa Umma (CHAUMA) saa 5:00 asubuhi, Chama cha Sauti ya Umma saa 5:30 asubuhi, Demokrasia Makini saa  8:30 Mchana na UPDP 8:30 Mchana  wanatarajiwa kuchukua fomu za uteuzi

 

 

Mawasiliano Yetu


Tume ya Uchaguzi Zanzibar

S.L.P 1001 - Zanzibar, Tanzania.

Simu: +255 242231489

Nukushi: +255 242233828

Mitandao ya Kijamii